Kwa dhati kabisa, simuoni mgombea wa akina Polepole kuwa na uwezo wa kukabili changamoto hizo. Ndio maana inabidi kurudi kwa Polepole kumuomba awajibu Wazanzibari masuala ya msingi. Maana yeye anayejinadi kuwa ataleta maendeleo ndiye kikwazo cha mwanzo cha mgombea wao.
Najiuliza: hivi tukifika Oktoba 28 na Maalim Seif bado mzima kasimama mbele yetu na kwenye kipande cha kura yumo, tutakimbilia wapi? Hivyo Kisiwandui sasa kumekuwa na Israel tu, hakuna tena akili za kupanga mikakati ya ushindi?
RAIS Ahmed Abdallah wa Comoro aliyeuliwa Novemba 26, 1989 na askari wa kizungu aliowakodi mwenyewe, anakumbukwa kwa mengi. Kuna wanaomuona kuwa shujaa kwa kuthubutu kuikabili Ufaransa na kutangaza kuwa Comoro ni … Continue Reading Muungano unalindwa kwa nguvu
Kijijini kwetu alikuwepo mzee mmoja ambaye alikuwa maarufu sana. Miongoni mwa mambo yaliyompa umaarufu ni jinsi alivyokuwa mweledi katika elimu ya dini ya Kiislamu kiasi cha kuwafundisha baadhi ya aalim … Continue Reading Masauni amelewa pombe gani?
Haftar anaishtumu serikali ya Tripoli kuwa imejaa magaidi na amekuwa akidai kwamba lengo lake ni kuwapiga vita magaidi wote wenye kufuata mielekeo mikali ya Kiislamu kama vile wafuasi wa Dola ya Kiislamu (Islamic State) au Al Qa‘eda. Amekuwa akishtumu kwamba wote wenye kuingiza dini katika siasa ni magaidi wakiwa pamoja n ahata wafuasi wa vuguvugu la Udugu wa Kiislamu (Jami’yat al Ikhwan al Muslimin).
Al Bashir hakuwa na uungwana huo. Aliipindua serikali iliyochaguliwa ya Waziri Mkuu Sadiq al Mahdi baada ya serikali hiyo kuanza mashauriano na waasi wa Sudan Kusini. Ajabu ya mambo ni kwamba miaka kadhaa baadaye mnamo 2005, al Bashir alifanikiwa kuvikomesha vita vya pili vya wenyewe kwa wenyewe na kuwezesha pafanywe kura ya maoni ambayo hatimaye iliigawa sehemu ya kusini iwe taifa huru la Sudan Kusini.
KATIKA maktaba yangu nina kitabu, kijitabu kwa hakika, chenye kufundisha namna ya kufanya mashambulizi ya kigaidi katika miji kwa lengo la kupindua serikali. Kinaitwa “Minimanual of the Urban Guerilla” na … Continue Reading Algeria: Darasa za bure barabarani