Haftar anaishtumu serikali ya Tripoli kuwa imejaa magaidi na amekuwa akidai kwamba lengo lake ni kuwapiga vita magaidi wote wenye kufuata mielekeo mikali ya Kiislamu kama vile wafuasi wa Dola ya Kiislamu (Islamic State) au Al Qa‘eda. Amekuwa akishtumu kwamba wote wenye kuingiza dini katika siasa ni magaidi wakiwa pamoja n ahata wafuasi wa vuguvugu la Udugu wa Kiislamu (Jami’yat al Ikhwan al Muslimin).
Al Bashir hakuwa na uungwana huo. Aliipindua serikali iliyochaguliwa ya Waziri Mkuu Sadiq al Mahdi baada ya serikali hiyo kuanza mashauriano na waasi wa Sudan Kusini. Ajabu ya mambo ni kwamba miaka kadhaa baadaye mnamo 2005, al Bashir alifanikiwa kuvikomesha vita vya pili vya wenyewe kwa wenyewe na kuwezesha pafanywe kura ya maoni ambayo hatimaye iliigawa sehemu ya kusini iwe taifa huru la Sudan Kusini.
KATIKA maktaba yangu nina kitabu, kijitabu kwa hakika, chenye kufundisha namna ya kufanya mashambulizi ya kigaidi katika miji kwa lengo la kupindua serikali. Kinaitwa “Minimanual of the Urban Guerilla” na … Continue Reading Algeria: Darasa za bure barabarani