Utamaduni na Fasihi
Mwanangu unanijia, hali unatiririka, damu muili mzima
Tumboni ninaumia, machango yanikatika, moyo wapwita; wauma
Lipi limekutokea, shenzi walolaanika, washakupiga kwa vyuma?
Kwa nini wamekupiga? Endelea kusoma shairi hili.
Niende wapi kwa nani, nikapate haki yangu?
Nani wa kunithamini, wa kujuwa utu wangu___
Ikiwa mahakamani, ndipo ninyimwapo changu
Ni wapi hapo pengine? Endelea kusoma shairi hili
Ushavyoila ndoana, papa huna ushupavu
Hata ukawanawana, kwa vishindo na maguvu
Ndoana ishakukwama, huna tena uwerevu
Na kila tukivutana, ndipo twakuzidi nguvu
Zama za kufa zikija:
Zije ningali ni mtu, sijageuka nguruwe
Sijakuwa nyama mwitu, azaaye na wanawe
Zije bado nina utu, hiondoka nililiwe
Hishima tuwe pamoja.
Juwa lenda machweoni
Linazama baharini
Dhahabu yake launi
Na mvuvi kidauni
Arudi toka mavuvi
Ungalinipa dhahabu, almasi na yakuti
Na makasiki ya fedha, na mabakuli ya wati
Kwa kutaka niiwache, Zenji yangu siiwachi
Ni radhi utwae yote, lakini si kitu hichi
Kwamba ndiyo roho yangu!
Madhali hatujataka, hatunyanyuki, tungawa wa kunyanyuka
Tungawa wa kunyanyuka, hatuinuki, tupaswapo kuinuka
Tupaswapo kuinuka, hatujishiki, sababu ya kutotaka
Zama za kuja kutaka, za kutaka jiinuwa, ‘tajiinuwa wenyewe.
Wataamka, nasema wataamka, nalo nelisema kale
Wataamka, punde muda ukifika, kwanza wawache walale
Wataamka, kwa majogoo kuwika, na jua kuvya mishale
Wataamka, kwa kwisha kupambazuka, na kwa kwisha tongo zile!
Kuna yapi ya uchungu, kama kumwagiwa damu?
Ya watoto damu changa, ‘liyotarajiwa
Ya vijana damu mbichi, ‘liyotegemewa
Ya wazazi damu pevu, ‘liyohishimiwa
Tukufu damu kumwagwa, pasipo ubinadamu
Ya mabavu serikali, watawala madhalimu
Wadhulumu watu wangu
Lakini, kesho, kwa jina Mungu___
Tutainuka, tupambane hadi ushindi!
Kwa jinalo wewe, tungo nayandika, na kuikariri
Hitaka ujuwe, ndiwe mtukuka, ndiwe wangu huri
Sina mwenginewe, wala hatazuka, wa kumkubali
Wat’ani ni wewe, kila kitu wewe, Mama Zinjibari!
Bwanatosha shukrani, mwanao kunijuliya
Tupoe sote wendani, Watani yakwangamia
Mbele ya zetu uyuni, mambo yatuharibikia
Ndilo niloshuhudia, nilipokwenda nyumbani
Natamani pumzika, hizi balaa
Yanipungue mashaka, kunilemea
Natamani kuushika, kuung’ozoa
Ungekuwa wa kung’oka, ningeung’oa!
Hutwaa mizani, kupima utukufuwo
Hwenda chini, mno sana upandeo
Ile ya thineni, yenye tele mashindio___
Haiji chini, ni mkubwa uzitowo
Mi’ sipaoni, ushudupo mfanowo
Nife leo ama kesho, ndanimo nanichimbiwe ufuwo!
Ulipopata BUNDUKI:
Hukukaa msituni
Bali wekaa mjini
Kwenye raha kila fani
Soda, kuku na Pajero!
Kwatakwata na mdundo, punda jasho lakutoka
Punda wenda kwa kishindo, mwendo mchaka mchaka
Mgongoniko ni rundo, bahasha la taka taka
Na bwana fimbo kashika, punda uongeze mwendo
1.Haya! Kuwa ongezeka, jipe nyadhifa na vyeo
Jifanye umetukuka, kwa deko, ringo na shoo
Bali utavyotanuka, juwa una hatimayo
Yangakuwa maguuyo, mawingu hutayafika
1. Naandika kwa kilio, machozi hadi viatu
Wino ndilo kimbilio, na shahidi Mola wetu
Nayawahi haya leo, bado ningalithubutu
Naliwahi hili bao, bado lingali ni letu
Sababu hatuna chetu, vyote vishakuwa vyao
UHAKIKI WA KITABU CHA ‘JUMBAMARO’ I
“Kwangu mimi, nyumbani huku anakotaka kurudi Bwan’ Said hakuna tafauti kubwa na kulivyo hapa nyumbani, Zanzibar. Zanzibar ya sasa ina mambo yako shaghala baghala kama yalivyo ndotoni kwa Bwan’ Said. Maadili yanaporomoka kwa kasi kubwa mno na, ninaposoma hadithi hii ya “Msafiri”, nashindwa kuzizuia fikira zangu zisizivute picha za Kibanda Ugali (Kiwengwa), New Happy Lodge (Mji Mkongwe) au hata maeneo ya Golf, ambako kuna biashara ya tupu inayoendeshwa kwa siri ya wazi.” Endelea kusoma uhakiki huu.
UHAKIKI WA KITABU CHA ‘JUMBAMARO’ II
“Mjumbe aliyekuwepo Zanzibar alikuwa ni gazeti la Dira, ambalo lilikuwa limejitolea kuandika na kuchambua ukweli kuhusu masuala mbali mbali ya kijamii, kiuchumi na kisiasa ambayo yalihusu hatima ya Zanzibar. Lakini hilo halikuwafurahisha mabwana wa Zanzibar, na matokeo yake ni kuwa liliandamwa hadi likafungiwa moja kwa moja, huku wahusika wake wakitangazwa kuwa si raia wa nchi hii. Hapa nazungumzia Mzee wangu, Ali Nabwa, ambaye amegeuzwa mkimbizi katika nchi ya mababu na mabibi zake. Ni huzuni iliyoje kwamba hata alipokuwa anakiwekea utangulizi kitabu hiki tunachokichambua hapa, alilazimika kusaini kama TX, yaani mfanyakazi kutoka nje ya nchi. Mjumbe kaemewa” Endelea kusoma uhakiki huu.
Waliotutangulia
Nchi wakatuachia
Na wanaofuatia
Wajibu kuikutia.
Ndipo kwa huo wajibu
Tungo hii nakutubu
Iwe nayo ni sababu
Ya Watani kulindia
TAFADHALI BONYEZA HAPA KUCHANGIA MAONI YAKO. UNASHAURIWA KUANDIKA MADA YA KILE UNACHOKICHANGIA.


