jump to navigation

Ajali ya meli: Maalim Seif azitaka mamlaka ziwajibike May 30, 2009

Posted by Mohammed Khelef Ghassani in Politics.
1 comment so far

Na Salma Said, Zanzibar

Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, amezitaka mamlaka za usafirishaji na mawasiliano chini zilizo chini ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) kuwajibika ili kuipa heshima serikali ya Amani Karume mbele ya umma kutokana na uzembe uliopelekea kutokea kwa ajali ya Meli ya MV Fatihi jana usiku kisiwani Unguja.

Kwa kauli hii, bila shaka, Maalim Seif anamgusa moja kwa moja Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi wa SMZ, Machano Othman Said, akimtaka aanze kujiuzulu wadhifa wake akifuatiwa na maafisa wengine katika mamlaka husika.

Maalim Seif ametoa tamko hili leo mara baada ya kutembelea eneo la ajali na kupata maelezo mafupi toka kwa maofisa wa Shirika la Bandari la Zanzibar, akiwemo Mustafa Jumbe ambaye ni mkurugenzi wa shirika hilo.

Maalim Seif amesema ni jambo la kusikitisha kuona hata taarifa za usafirishaji abiria zikiwa hazifahamiki wala idadi ya abiria waliokuwemo ikikanganya akili na zaidi meli hiyo inaaminika ilikuwa mbovu.

Katibu Mkuu huyo wa CUF alisema siku chache zilizopita meli hiyo ilikuwa ikitoka Pemba na kulazimika kushusha abiria bandari ndogo ya mkokotoni kabla ya kutia nanga katika bandari ya Maalindi na hadi sasa haijaelezwa wazi kama tatizo lilikuwa nini na kisha ianze kubeba tena abiria.

“Vyombo vilivyo husika vilichukua hatua gani ya kuhakikisha meli hii sasa ni nzima na inafaa kuchukua tena abiria na kusafiri majini,tuna mashaka pengine mamlaka husika hazikuchukua hatua sahihi.”

Aidha ameilalamikia hatua ya meli hiyo kupata ajali ikiwa bandarini lakini zikakosekana juhudi za haraka za kitaalam za kuokoa maisha ya abiria na mizigo yao na mamlaka zinazohusika kutojaribu kunusuru hali hiyo ya taharuki.

“Hata pale walipotokea wasamaria wema waliokuwa tayari kutaka kujitolea kusaidia kutokana na uzoefu walionao walikatazwa na hivyo kuchukua muda wa takriban saa nane hadi wazamiaji kutoka kikosi cha KMKM kufika bandarani.”

Katibu Mkuu huyo wa CUF amesema hiyo ni hatari katika nchi na jamii ingetazamia sana kuwepo kwa kikosi kilichoandaliwa vyema kimafunzo kwa masjanga ya uokoaji hapo bandarini kusaidia kulihami janga hilo .

“Tunaiotoka serikali kwanza ichukue hatu za dharura ili kuhakikisha hakuna mtu aliyebaki, na kama kuna maiti zipatikane na familia zao wakazike, mamlaka zinazosimamia usafiri ziwajibike na usalama wa vyombo ufahamike kabla ya kuanza safari katika kubeba abiria na mizigo.”

Aliongeza kusema kuwa kuyafumbia macho masuala kama hayo wakati wake umepita na sasa ni lazima wanaohusika wawajibike ili kujenga nidhamu ya uwajibikaji kutokana na dhamana walizobebeshwa na serikali.

Hata hivyo, Maalim Seif alisema Serikali ya Muungano pia ilitakiwa iweze kusaidia kutoa misaada yao, lakini hakuna dalili za serikali hiyo kushiriki katika uokoaji huo.

Wakati akiondoka bandarini, Rais Karume aliulizwa serikali yake inachukua juhudi zipi alisema hata wapinzani nao ni sehemu ya serikali hivyo haiyumkini kuuliza serikali inachkua hatua gani kwa sasa.

“Serikali ina mamlaka zake. Majumuisho wake ndiyo unapata serikali. Kila mtu ni serikali hata wewe mwandishi ni serikali. Hata hawa wapinzani.” (huku akimuonyesha kidole chake Maalim Seif kuwa ni sehemu ya serikali).

Rais Karume na Maalim Seif, wote, kwa nyakati tofauti, walitoa salamu za pole kwa wafiwa na kuwatakia majeruhi wote katika ajali hiyo wapate uzima haraka ili washiriki katika kazi za kimaendeleo.

Meli yazama Zanzibar May 30, 2009

Posted by Mohammed Khelef Ghassani in Politics.
add a comment

Na Salma Said, Zanzibar

MELI ya mizigo ya inayomilikiwa na Kampuni ya Seagul, MV Fatih, imepinduka na kuzama katika Bandari ya Malindi, Zanzibar, usiku wa kuamkia jana huku maiti za watu watatu zikiwa zimepatikana zikielea na watu wengine 27 wamejiokoa katika ajali hiyo na mamilioni ya mali kupotea.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, Bakari Khatib Shaaban amethibitisha kutokea kwa vifo hivyo ambapo alisema kwamba Meli hiyo ilikuwa tayari imeshafunga gati katika Bandari ya Malindi majira ya saa 4.00 kamili uski juzi usiku na abiria waliokuwemo walikuwa wanataka kushuka lakini ghafla ilipinduka na kuzama baharini.

Kamanda Shaaban alisema hadi jana mchana ni maiti za watu watatu tu ndizo zilizoonekana ikiwemo ya mtoto mdogo wa kiume, na watu wazima mwanamke na mwanaume ambao hawakuweza kufahamika majina yao kamili kutokana na hakna jamaa waliozitambua maiti hizo.

Waliookolewa katika ajali hiyo ni Machano Mkinai, mkaazi wa Mkwajuni na Kitiba Mussa Kitiba, Gamba mkoa wa Kaskazini Unguja, Halima Mussa wa Arusha, Hassan Omar, Maulid Abdalla, wote wa Kisiju Mkoa wa Pwani.

Wengine ni Fatma Ali Salum, wa Kinyasini Wete kisiwani Pemba, Hawa Juma Saleh wa Rukwa Tanzania Bara, Zainab Ali Kitiba, Tandale Dar es Salaam, Sharifa Hamad wa Wingwi Pemba, Ramadhan Juma Mohammed Tandale na Omar Khamis Mohammed wa Vinguguti Dar es Salaam.

Amesema baada ya kutokea tukio hilo polisi walitaka maelezo ya Nahodha wa Meli hiyo, Ussi Ali ambaye wanamshikilia kwa maelezo zaidi lakini lakini maelezo yake yanaonesha wasi wasi kwa jeshi la polisi kutokana na kuwepo utatanishi mwingi katika maelezo ya Nahodha huyo.

Kamanda Shaaban alisema kwamba awali Nahodha alisema katika meli yake kulikuwa na abiria 25 na wafanyakazi 13, lakini Polisi inatilia shaka taarifa hizo kwani yawezekana Meli hiyo ilibeba abiria wengi na mizigo hivyo wanaendelea kumhoji Nahodha huyo hadi hapo maelezo jeshi la polisi litakapopata maelezo ya kuridhisha kutoka kwa Nahodha huo.

“Jeshi la polisi halijaridhishwa na maelezo ya Nahodha bado hasa katika idadi za abiria alizozitoa lakini bado tunaendelea kumuhoji kwani hatujaridhika na taarifa yake” Alisema Kamanda huyo.

Kamanda Shaaban alisema jeshi la polisi bado na uchunguzi wa kina ili kujua chanzo cha ajali hiyo na haitosita kuwachukulia hatua wanaohusika na kuwataka wananchi kutulia na kuacha vyombo vya sheria kufanya kazi zao kwa wazi.

Hali katika Bandari ya Zanzibar baada ya ajali hiyo kutokea ilionekana kuwa katika kitahanani kikubwa kwa wananchi wakiwemo wafanyabiashara waliokuwa eneo hilo wakisubiri mizigo yao na jamaa zao jambo ambalo lilisababisha msongomano mkubwakiasi cha kuwafanya Polisi kuwatawamya kwa kurusha risasi hewani.

kuwapo kwa hali hiyo kulilifanya Jeshi la Polisi kuweka doria kali katika maeneo yote huku wakishirikiana na baadhi ya askari wa vikosi vyengine kutokana na baadhi ya vibaka kujipenyeza na kuanza kuvuna mali zilizokuwemo katika Meli hiyo.

Hata hivyo kazi za utafutaji wa maiti nyengine iliendelea kwa siku nzima ya jana baada ya wazamiaji zaidi ya 30 wa KMKM kuifanya kazi hiyo baada ya kuwasili saa 8.00 za usiku wa juzi.

Kazi hiyo baada ya kupatikana kwa maiti tatu ilisita kwa usiku huo na kuendelea tena jana asubuhi kuanzia saa nne ambapo waokoaji hao waliamua kutumia mbinu mbali mbali za kuwawezesha kuingia ndani ya meli hiyo lakini hadi saa saba mchana walikuwa bado hawajafanikiwakuingia ndani ya meli hiyo.

Akisimulia mkasa wa ajali hiyo kepteni aliyekuwa akiendesha meli hiyo, Ussi Ali Ussi, alisema wakati akiingia Bandarini ghafla aliona meli hiyo ikijaa maji na kulala upande wa kushoto.

Alisema alianza safari yake saa 10.00 kutoka Dar es Salaam na kuja Unguja ambapo aliwasili saa 3.30 usiku lakini akiwa njiani alipata tatizo la usukuni kutoenda vizuri akiwa karibu na kufika Bandarini hapo.
Akiendelea alifahamisha ndani ya meli hiyo alibeba mizigo yenye uzito watani 40, abiria 25 na wafanyakazi wake walikuwa ni 13 ambapo watatu aliwaona baada ya meli hiyo kuzama lakini kwa wakati huo wa usiku hakujua wapi walipo.
Rais wa Zanzibar Amani Abeid Karume, Waziri Kiongozi wa Zanzibar, Shamsi Vuai Nahodha na Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad ni miongoni mwa viongozi waliofika katika eeo la bandari na Zanzibar kuonana na abiria waliookolewa na kushuhudia ajali hiyo.

Rais Karume aliwataka mafundi wanayoifanyakazi ya uokozi kuonakuwa wanajitahidi kuhakikisha kuitafuta miili zaidi kama bado imo ndani ya meli hiyo.

Katika bandari hiyo umati kubwa ulikuwa umesheheni huku mamia ya watu wakiwa wamekaa nje ya geti la gati wakitaka kuingia ndani kushuhudia jamaa zao na ajali hiyo ambayo jambo ambalo limesababisha msongamano mkubwa bandarni hapo.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bandari Zanzibar, Mustafa Aboud Jumbe alimweleza Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Shamsi Vuai Nahodha kwamba juhudi za uokoaji inaendelea kwa kushirikiana na Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo (KMKM), Polisi na wadau wengine wanaojitolea kusaidia uokozi huo.

Jumbe alisema bado ni mapema kuielezea serikali juu yahatua za kuweza kuchukuliwa zaidi kwa vile wameanza kuifanya kazi hiyo ambapo imekuwangumu kutokanana na meli hiyo kuwa na mzigo mkubwa kiasi ambacho kimekuwa kikiwapa usumbufu waokowaji.

Kutokana na kuwepo kwa umma wa wananchi katika eneo la bandari Shirika la Bandari liliamua kufunga milango yake yote ya Bandari hiyo kwa usalama wa watu huku waandishi wa habari wakipata kazi kubwa katika ufanyaji kazi zake kutokana na vikwazo walivyokuwa wakiwekewa katika eneo hilo.

Jumbe alisema kwamba baadae watajaza upepo Meli hiyo iliyozama kwa kutumia kifaa maalum ili mizigo na watu waliokuwepo waweze kuja juu ambapo kazi hiyo itafanywa baada ya maji kujaa kwani kwa wakati huo maji yalikuwa yanakupwa na kazi hiyo ingeshindikana kufanyika.

Waziri Kiongozi aliwataka Viongozi wa Bandari kuieleza Serikali ni msaada gani wanaohitaji ili kuweza kufanikisha uokoaji wa mizigo, watu na meli hiyo ambapo Shirika la Bandari lilisema limejipanga vyema kukabiliana na janga hilo.

Wakati shirika la bandari likitoa ahadi hiyo hadi sasa hakuna msaada uliopatikana wa kutoa maiti zilizokuwa ndani ya meli hiyo huku Rais wa Zanzibar akilitaka shirika hilo kuomba msaada shirika la bandari la dare s salaam kuja kusaidia kuwaokoa watu waliomo ndnai ya meli hiyo.

Habari zaidi kutoka kwa abiria walionusurika katika ajali hiyo wamedai kuwa ndani kulikuwa na watu wengi wanaokisiwa kufikia 100, lakini Nahodha wa Meli hiyo anapingana na idadi hiyo na kusisitiza kwamba meli yake ilikuwa na idadi ndogo ya abiria.

Halima Mussa mkazi wa Arusha ambaye amenusurika katika ajali hiyo alisema kwamba wakati tukio hilo linatokea alikuwa tayati ameanza kushuka ndani ya Meli hiyo, lakini ghafla aliona ikipinduka wakati ikiwa imefunga gati na baadae akiwa katika maji alijikuta ameshikilia kitu.

“Mimi namshukuru Mungu kwa sababu nilikuwa nashuka lakini ghafla nikajikuta nimo katika maji lakini baadae nikakamata kitu bila kukijua ni kitu gani nilichoshikilia na nikaaza kupiga mayowe ya kutaka msaada na huku nyuma yangu nasikia sauti nyengine watu wakiomba msaada kuna watu wlaiokuwepo katika maji ndio wakanisaidia kwa kunambia shikilia hivyo hivyo hicho kitu na kunitaka ninyoosha mikono ndio waliponiokoa na kunileta juu” alisema huku akihema Halima Mussa.

Watu waliofika katika bandari ya Malindi yameilaumu serikali kw akshindwa kushukua hatua za dharura za kuweza kukabiliana na shughuli hiyo ambapo ajali imetokea majira ya saa 4 usiku lakini hadi saa tisa ndipo waokoaji waliopofika huku wakiwa hawana vifaa vya uokoaji.

“Ni dharau za hali ya mwisho hii maana ajali tokea saa 4 usiku lakini hawa watu wa KMKM wanakuja sa 9 hawana chochote cha kuweza kuwasaidia kuokoa abiria matokeo yake wamekuja na kuondoka kwa kisingizio cha kuongojea maji yakupwe” amesema Ali Haji Mkaazi wa Jangombe ambaye ana jamaa yake katika meli hiyo.

Naye Kepteni Juma wa meli ya Sea Bus amesema ipo haja ya kuwa na timu nzuri ya waokoaji na diver ili waeze kuwaokoa watu pindipo inapotokea ajali kama hiyo kwani.

“Lazima tuwe na timu nzuri ya divers wasaidie kuokoa lakini pia tax force ni muhimu kuwepo kwa ajili ya maafa kama haya na kufuata madili ya kazi ni kitu cha lazima kwa sisi manahodha ili kunusuru maisha ya watu” alisema Kemteni huyo.

Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad aliwaambia waandishi kwamba alisema wakati umefika hivi sasa kuhakikisha inalifanyia kazi tatizo hilo ambalo linaweza kuathiri wananchi wengi kwa kuziwajibisha taatisi husika kwa vile meli hiyo tayari hapo awali ilipata hitilafu na kulazimika kushusha abiria katika Bandari ya Mkokotoni baada kupata maharibiko ikitokea Pemba.

maalim Seif alisema ipo haja kwa serikali hivi sasa kuvifanyia ukaguzi vyombo vya usafiri kwa kuona inatenganisha huduma kati ya vile vinavyotoa huduma baharini.

Meli hiyo ambayo inamilikiwa na Said Mbuzi imeelezwa kuwa ilibeba mizigo mbali mbali ikiwemo Trekta, gari mbili, magunia ya unga wa ngano, sukari, mchele, magunia ya viazi, ya nyanya, mifuko ya saruji, magodoro na bidhaa nyengine ambazo zote zimezama huku wajanja wakitumia nafasi hiyo kuopoa bagodoro na bidhaa nyengine na kukimbia nazo nchi kavu.

Tukio za kuzama kwa Meli hiyo ambayo uzamaji wake unafanana sana na ule wa MV Bukoba linatokea wiki moja tu katika kumbukumbu ya kuzama kwa MV Bukoba mwezi Mei mwaka 1999 ambapo watu kadhaa walifariki dunia na kweka historia ya Tanzania katika ajali mbaya za meli zilizowahi kutokea nchini.

Qauli ya Umoja wa Wazalendo Kukhusu Msiba wa Kuzama Meli hapo Bandarini Malindi, Zanzibar; taarikhi 29.05.09. May 30, 2009

Posted by Mohammed Khelef Ghassani in Politics.
add a comment

Wazee wetu, Ndugu zetu,

Assalaam Alaaykum,

UMOJA, UHURU, UADILIFU

Qauli ya Umoja wa Wazalendo Kukhusu

Msiba wa Kuzama Meli hapo Bandarini

Malindi, Zanzibar; taarikhi 29.05.09.

Umoja wa Wazalendo, una wingi wa huzni kwa msiba uliotokea usiku wa jana, taarikhi 29 May, 2009; kwa kuzama meli hapo bandarini Malindi na kusababisha vifo, kupotea mali na kusababisha mashaka kwa abiria na kila aliekuwepo wakati huo. Haya ni maqadiri ya Mwenyezi Mungu Mtukufu Subhaanahu wa Taáala, linaloandikwa halizuiliki kutokea; bali lina sababu.

Hapana shaka huu ni msiba wetu sote, msiba wa kila Mzanzibari, ni msiba wa kila Muumini na kila binaadamu.

Tunamuomba Mwenyezi Mungu Mtukufu Subhaanahu wa Taáala awaghufirie makosa yao marehemu wetu, awalaze mahali pema, awatie Peponi kwa Rehma Zake, wao na jamii ya Waumini; na awazidishie subira na mapenzi wafiwa wote, Aamyn.

Huu ndio mwisho wetu sote, tunamuomba Mwenyezi Mungu Mtukufu Subhaanahu wa Taáala atujaalie mwisho mwema, sisi na jamii ya Waumini; Aamyn.

Mkono wetu wa taáazia tunaupeleka kwa Rais wa Zanzibar, Mhishimiwa Rais Aman Abeid Aman, Sirikali ya Zanzibar na wananchi wa Zanzibar kwa jumla.

إنّا لله و إنّا إليه راجعون

Mwenyezi Mungu Mtukufu Subhaanahu wa Taáala awajaalie marehemu wetu hawa ni miongoni mwa Mashahidi, Aamyn.

Wa Billahi Tawfiiq

Umoja wa Wazalendo

Zanzibar

May 30, 2009

Being a Zanzibari May 30, 2009

Posted by Mohammed Khelef Ghassani in Politics.
2 comments

* By Mohammed Saleh

What aspects of your background permit you to define yourself as a Zanzibari?

• Zanzibar being the country of my by birth and a land where my umbilical cord is lying
• Zanzibar being the country where my parents were born and grew up. The country where in some ways they have contributed towards its development
• Zanzibar being the country where there are numerous tombs of members of my extended family
• Zanzibar being the country where I grew up and received my basic religious and secular education
• Zanzibar being the country that I could identify with, in many ways, and that I could easily articulate on its various aspects
• Zanzibar being the country that consciously and/or unconsciously, objectively and/or subjectively attached with and could dream about and even become nostalgic of
• Zanzibar being the country that I could be proud of, that I could be sentimental with and going even as far as sacrificing my time, energy and even the best part of my life for its development and social welfare of its people
• Zanzibar being the country where I could be discriminated against and considered alien by those who are more alien than anybody else, but where I could naturally have the courage to resist without any hesitation against the racist bunch
• Zanzibar being the country where I could really and genuinely feel at home and at ease
• Zanzibar being the country where I could find and recall various aspects of my childhood and find my playmates, school mates, etc.

2. In what ways does your upbringing, language, culture, class, religion (or sect), physical environment, legacy, confirms this identification:
• Upbringing: It is one of the fundamental factors confirming my Zanzibari identity. My upbringing in a coastal cosmopolitan Zanzibari society had a major impact in the formulation and development of my system of representation. Despite living abroad for many years, integrating in the process many other non Zanzibari socio-cultural elements, the basis of my system of representation remains essentially Zanzibari. It continues to date to influence in some ways my socio-cultural orientation and world outlook. Through my Zanzibari upbringing, I was made to understand life in all its complexities, and to cherish honor and pride. These are some of the ideals that are highly valued by the society that one might find elsewhere, but for me, they reflect my Zanzibari identity.
• Language: I consider this an important element of my Zanzibari identity allowing me to differentiate with other Swahili speaking communities in many ways, including accents and colloquial. This is also true to the language used in Zanzibari literature, which I could identify with and feel part of it, allowing my assertion to the Zanzibari identity.
• Culture: Being part and parcel of the plural coastal societies of East Africa, with a number of socio-cultural similarities, my Zanzibari identity remains relevant by the existence and the performance of a number of customary rites, traditional and moral teachings giving room to some kind of differentiation with other non Zanzibaris. The inculcation of the following norms and values – principal moral foundation of Zanzibari, Swahili identity and culture further confirms my Zanzibari identification: respect (heshima), good behavior (adabu), honesty (uaminifu), ethics (uadilifu) and honour (ari).
• Class: This factor does not seem to have any particular importance and to play any role in my identification to Zanzibar, hence to my Zanzibari identity
• Religion: It forms an important part of social and moral background of my Zanzibari identity. Although, I am un-practicing Muslim but Islamic elements acquired through my Zanzibari upbringing still have a major impact in my world outlook and my daily life. However, I always make a difference between the Islamic religious practice that I grew up with in Zanzibar and those of elsewhere or the radical Islam. While talking about Islam in terms of Zanzibari identity, I put particular emphasis on tolerance. As a religion that came by dhow, and not imposed by sword, through trade, social and cultural interaction Zanzibar has been for many years characterized by religious tolerance. Zanzibari Islam has been all along open, tolerant and respectful of minority rights, including homosexuals. These elements contribute in my determining of my Zanzibari identity and in my differentiation with other Non Zanzibari Muslims or present Radical Zanzibari Muslims.
• Physical Environment (architecture, urbanity, countryside, etc): These factors play a particular role in my taste and appreciation of physical environment of the foreign countries that I am visiting or choose to visit. The Zanzibari architectural background, aspects of Zanzibari urbanity and even countryside consciously or unconsciously remain as my major reference points of appreciation or comparison. In this sense while appreciating and comparing the above elements through the Zanzibari lenses I am affirming my Zanzibari background and by rebound my Zanzibari identity.
• Legacy: Although identity is not static and is constantly being negotiated, most of the above mentioned elements remain to date valid and will take time to disappear. They remain the fundamental elements of what I could consider as part of my Zanzibari cultural legacy and identity. They are the elements that I could hardly replace but which I could very well, consciously or unconsciously, enrich with other socio-cultural elements of the foreign society that I am living in.
Other

3. In what ways these aspects hinder your identification (if any?)

None of these aspects hinder my identification. On the contrary, they are the fundaments providing the intellectual basis for the struggle against cultural hegemony and the efforts of those who are creating confusion among the people in terms of their Zanzibari, Swahili identity and language.

4. Please add any other issues you think would be of interest:
• Grew up in a Zanzibari cosmopolitan background facilitated a great deal and made me feel very much at ease mingling with people from other countries with similar plural background or not. For me identifying with Zanzibar goes even further to include a larger Swahili cosmopolitan coastal identity. For Zanzibar belongs to a larger Swahili plural identity of which I am attached and identify with.

5. Actions speak louder than words. While I tend to agree with all that has been suggested above, I also strongly believe that a true and committed Zanzibari should also be an activist one who is prepared to stand up and be counted for what he/she believes in or else he/she will fall for anything. Consequently, it is time for such Zanzibaris to support ZIRPP by actions rather than words; because it is only through ZIRPP that a discriminated and alienated Zanzibari could make the maximum use of his/her natural courage to resist without any hesitation against racial discrimation in all its forms and manifestations.

* My apology to Mr Mohamed Saleh who owns this article. I unknowingly published it with Muhammad Yussuf’s name. Mohammed Ghassany

Askari wauawa wakiwa lindoni May 26, 2009

Posted by Mohammed Khelef Ghassani in Politics.
add a comment

Na Ali Suleiman, Zanzibar

ASKARI wawili wa Kikosi cha Valantia (KVZ) cha Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
Bw.Juma Mcha Ali (25) pamoja na Bw. Taibani Mikidadi Ali (23), wameuwawa na majambazi wakiwa lindoni katika kituo cha mafuta Mwanakwereke. Majambazi hao hata hivyo hawakufanikiwa kupora fedha lakini walichukuwa silaha aina
ya RF ikiwa na risasi kumi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, Bw. Bakari Khatib Shaaban, alithibitisha
kutokea tukio hilo saa mbili usiku wa kuamkia jana na kusema majambazi hao, walivamia kituo hicho kwa lengo la kupora fedha.

Katika purukushani hizo, majambazi hao walifanikiwa kufyatua risasi na kuwauwa askari hao waliokuwa lindoni kwa kuwapiga risasi kichwa na kifuani.Baada ya hapo, walipora bunduki moja na kutoweka.

Kutokana na tukio hilo, Jeshi la Polisi mjini hapa linamshikilia Bw. Gideon Simponda kwa mahojiano, baada ya kukiri kumiliki gari namba ZNZ 634 lililohusika kwenye tukio hilo la ujambazi.

“Jeshi la Polisi linamshikilia, Bw. Gideon Leornard kwa uchunguzi zaidi…yeye alijitokeza na kusema anamiliki gari lililohusika kwenye tukio hilo na kutelekezwa na majambazi hayo,” alisema Kamanda Shaaban.

Alisema baada ya kufuatilia, Polisi walifanikiwa kupata bunduki iliyoporwa na
majambazi hao. Kamanda Shaaban alisema majambazi hao pia walimjeruhi, Bw. Bilali Omar aliyekuwa akipita njia wakati wa tukio hilo.

Askari wa Vikosi vya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar hutumika kwa ajili ya kulinda
vituo mbalimbali vya mafuta pamoja na taasisi zingine, watu binafsi na
mabenki.

Kamanda Shaaban alisema, Jeshi lake linaendesha msako mkali kuwanasa majambazi hao.

Chanzo: Majira