Kipanga cha Muhammed Seif, Januari 27 na makinda ya kunguru weusi wa Zanzibar January 23, 2008
Posted by Mohammed Khelef Ghassani in Politics.add a comment
Na Mohammed Ghassani
Nianze kwa kunukuu utungo niliouandika miaka saba nyuma, yaani Januari, 2001, katika wakati ambao mauaji dhidi ya raia wasiokuwa na hatia yakiendelea Unguja na Pemba. Tembelea mtandao wa Shirika la Haki za Binaadamu, Human Rights Watch, http://www.hrw.org/reports/2002/tanzania/zanz0402.htm, kujisomea mwenyewe namna unyama huo ulivyotekelezwa. Niliuita utungo huu ‘Ulipozipata Bunduki,’ na ilikuwa ni suto kwa utungo ‘Nikizipata Bunduki’ ulioandikwa na Muhammed Seif Khatib katika kitabu chake, Fungate ya Uhuru. (more…)
Kesho Tutainuka! January 18, 2008
Posted by Mohammed Khelef Ghassani in Culture.add a comment

La kulisema halipo, la kulifanya sinalo. Lakini dhamira yanisukuma, kuna siku yatakwisha. Heshima yangu itarudi na utu wangu utatambuliwa. Yalinipata kwa sababu ya Uzanzibari wangu, yataondoka kwa sababu ya Uzanzibari wangu. Ewe Mungu niongoze njia!
Kuna yapi ya uchungu, kama kumwagiwa damu?
Ya watoto damu changa, ‘liyotarajiwa
Ya vijana damu mbichi, ‘liyotegemewa
Ya wazazi damu pevu, ‘liyohishimiwa
Tukufu damu kumwagwa, pasipo ubinadamu
Ya mabavu serikali, watawala madhalimu
Wadhulumu watu wangu
Lakini, kesho, kwa jina Mungu___
Tutainuka, tupambane hadi ushindi! (more…)
Kwa Jina la Zanzibar January 18, 2008
Posted by Mohammed Khelef Ghassani in Culture.add a comment
Kwa jinalo wewe, tungo nayandika, na kuikariri
Hitaka ujuwe, ndiwe mtukuka, ndiwe wangu huri
Sina mwenginewe, wala hatazuka, wa kumkubali
Wat’ani ni wewe, kila kitu wewe, Mama Zinjibari! (more…)

