jump to navigation

Kipanga cha Muhammed Seif, Januari 27 na makinda ya kunguru weusi wa Zanzibar January 23, 2008

Posted by Mohammed Khelef Ghassani in Politics.
add a comment

Hivi ndivyo ambavyo vyombo vya dola vilivyowashughulikia 'kunguru weusi' wa Zanzibar mwaka 2005

Na Mohammed Ghassani

Nianze kwa kunukuu utungo niliouandika miaka saba nyuma, yaani Januari, 2001, katika wakati ambao mauaji dhidi ya raia wasiokuwa na hatia yakiendelea Unguja na Pemba. Tembelea mtandao wa Shirika la Haki za Binaadamu, Human Rights Watch, http://www.hrw.org/reports/2002/tanzania/zanz0402.htm, kujisomea mwenyewe namna unyama huo ulivyotekelezwa. Niliuita utungo huu ‘Ulipozipata       Bunduki,’ na ilikuwa ni suto kwa utungo ‘Nikizipata Bunduki’ ulioandikwa na Muhammed Seif Khatib katika kitabu chake, Fungate ya Uhuru. (more…)

Kesho Tutainuka! January 18, 2008

Posted by Mohammed Khelef Ghassani in Culture.
add a comment
La kulisema halipo, la kulifanya sinalo. Lakini dhamira yanisukuma, kuna siku yatakwisha. Heshima yangu itarudi na utu wangu utatambuliwa. Yalinipata kwa sababu ya Uzanzibari wangu, yataondoka kwa sababu ya Uzanzibari wangu. Ewe Mungu niongoze njia!

La kulisema halipo, la kulifanya sinalo. Lakini dhamira yanisukuma, kuna siku yatakwisha. Heshima yangu itarudi na utu wangu utatambuliwa. Yalinipata kwa sababu ya Uzanzibari wangu, yataondoka kwa sababu ya Uzanzibari wangu. Ewe Mungu niongoze njia!

Kuna yapi ya uchungu, kama kumwagiwa damu?

Ya watoto damu changa, ‘liyotarajiwa

Ya vijana damu mbichi, ‘liyotegemewa

Ya wazazi damu pevu, ‘liyohishimiwa

Tukufu damu kumwagwa, pasipo ubinadamu

Ya mabavu serikali, watawala madhalimu

Wadhulumu watu wangu

Lakini, kesho, kwa jina Mungu___

Tutainuka, tupambane hadi ushindi! (more…)

Kwa Jina la Zanzibar January 18, 2008

Posted by Mohammed Khelef Ghassani in Culture.
add a comment
Zanzibar, kwayo tumezaliwa na kwayo tutafia

Zanzibar, kwayo tumezaliwa na kwayo tutafia

Kwa jinalo wewe, tungo nayandika, na kuikariri

Hitaka ujuwe, ndiwe mtukuka, ndiwe wangu huri

Sina mwenginewe, wala hatazuka, wa kumkubali

Wat’ani ni wewe, kila kitu wewe, Mama Zinjibari! (more…)